sw_tw/bible/kt/judge.md

769 B

hukumu

Ufafanuzi

Neno "hukumu" mara nyingi humaanisha kufanya maamuzi kama jambo liko sawa kimaadili au kama haliko sawa.

"Hukumu ya Mungu" mara nyingi humaanisha uamuzi wake kulaani kitu au mtu muovu. Hukumu ya Mungu mara nyingi huhusisha kuwaadhibu watu kwa dhambi zao. Neno "hukumu" inaweza pia kumaanisha "kulaani." Mungu anawaagiza watu wake kutowahukumu wengine kwa naamna hii. Maana nyingine ni "uamuzi kati ya" au "kuhukumu kati ya", yaani kuchagua ni mtu gani yuko sahihi katika ugomvi kati yao. Katika mazingira mengine, "hukumu" za Mungu ni yale aliyeamua ni mema na yenye haki. Zinafanana na amri, sheria na maagizo yake. "Hukumu" inaweza kumaanisha uwezo wa busara wa kufanya maamuzi. Mtu anayekosa "hukumu" hana hekima kufanya maamuzi ya busara.