sw_tw/bible/kt/imageofgod.md

717 B

mfano wa Mungu, mfano

Ufafanuzi

Neno "mfano" inamaanisha kitu kinachofanana na kitu kingine au ni kama tabia ya mtu au asili yake. Neno "mfano wa Mungu" inatumika katika njia tofauti, kulingana na mazingira.

Katika mwanzo wa nyakati, Mungu aliwaumba binadamu "katika mfano wake", ambayo ni "kwa kumfanana." Hii inamaanisha kuwa binadamu wana sifa fulani zinazoonesha mfano wa Mungu, kama uwezo wa kusikia hisia, uwezo wa kufikiri na kuwasiliana, na roho inayoishi milele. Biblia inafundisha kwamba Yesu, Mwana wa Mungu, ni "mfano wa Mungu," kwamba yeye ni Mungu mwenyewe. Tofauti na binadamu, Yesu hakuumbwa. Kutoka milele yote. Mungu Mwana ana sifa zote za Mungu kwa sababu ana asili sawa na ya Mungu Baba.