sw_tw/bible/kt/hypocrite.md

964 B

Mnafiki, unafiki

Ufafanuzi

Neno 'mnafiki' humrejelea mtu ambaye hufanya mambo ili aonekane mwema, ingawa kwa siri hufanya mambo maovu. Neno 'unafiki' hurejelea tabia ambayo huwahadaa watu kwa kufikiri kuwa mtu huyo ni mwenye haki. Wanafiki wanapenda kuonekana wakiwa wanafanya mambo mazuri, hivyo watu hufikiri kuwa ni watu wazuri. Mara kwa mara watu wanafiki huwakosoa watu wengine kwa kufanya mambo yale yale ya dhambi ambayo wao wenyewe huyafanya. Yesu aliwaita Mafarisayo kuwa ni wanafiki kwasababu walifanya matendo ya kidini kama vile kuvaa aina fulani ya nguo na kula chakula fulani, lakini hawakuwa wema na wenye haki kwa watu. Mtu mnafiki huweka wazi makosa ya watu wengine, lakini yeye mwenyewe hakubali makosa yake.

Mapendekezo ya tafsiri Baadhi ya lugha huwa na maneno kama "sura mbili" ambayo hutumika kumrejelea mnafiki au matendo ya mnafiki. Namna nyingine ya kutafsiri neno mnafiki ni "mdanganyifu, mtu anayejifanya, mwongo,"