sw_tw/bible/kt/highpriest.md

728 B

kuhani mkuu

Ufafanuzi

Neno 'kuhani mkuu' hurejelea kuhani maalumu aliyekuwa ameteuliwa kutumika kwa mwaka mmoja kama kiongozi wa makuhani wote wa Wayahudi. Kuhani mkuu alikuwa na majukuu mahususi. Alikuwa ni mtu pekee aliyeruhusiwa kuingia mahali patakatifu sana katika hekalu ili kutoa sadaka maalumu mara moja kwa mwaka. Waisraeli walikuwa na makuhani wengi sana, lakini walikuwa na kuhani mkuu mmoja kwa muda fulani. Kipindi alichokamatwa Yesu, Kayafa alikuwa kuhani mkuu. Anasi, Baba mkwe wa Kayafa anatajwa mara kadhaa kwasababu alikuwa kuhani mkuu hapo awali, huenda alikuwa bado na mamlaka na nguvu fulani juu ya watu.

Mapendekezo ya tafsiri 'Kuhani mkuu" tunaweza kutafsiri kama "kuhani wa daraja la juu"