sw_tw/bible/kt/godthefather.md

1.0 KiB

Mungu Baba, Baba wa mbinguni, Baba

Ufafanuzi

Misemo, "Mungu Baba" na "Baba wa mbinguni" ina maana ya Yahwe, Mungu mmoja wa kweli. Msemo huu hujitokeza kama "Baba" haswa pale Yesu anamaan ya yeye.

Mungu alikuwepo kama Mungu Baba, Mungu Mwana, na Mungu Roho Mtakatifu. Kila mmoja ni Mungu kamili, na bado wote ni Mungu mmoja. Hii ni siri ambayo binadamu wa kawaia hawezi kuelewa kikamilifu.

Mungu Baba alimtuma Mungu Mwana (Yesu) duniani na yeye humtuma Roho Mtakatifu kwa watu wake.

Yeyote anayemwamini Mungu Mwana anakuwa mtoto wa Mungu Baba, na Mungu Roho Mtakatifu huja kuishi ndani ya mtu huyo. Hii ni siri nyingine ambayo binadamu hawawezi kuelewa kikamilifu.

Mapendekezo ya Tafsiri

Katika msemo "Mungu Baba" ni bora kutafsiri "Baba" na neno sawa ambalo lugha hutumia kikawaida kumaanisha baba wa kimwili.

Msemo "Baba wa mbinguni" unaweza kutafsiriwa na "Baba anayeishi mbinguni" au "Baba Mungu ambaye anaishi mbinguni" au "Mungu Baba kutoka mbinguni".

Kawaida "Baba" inaandikwa kwa herufi kubwa, kuonyesha ya kwamba hii inamaanisha Mungu.