sw_tw/bible/kt/godly.md

555 B

utauwa, utauwa

Ufafanuzi

Msemo "utauwa" unatumika kumwelezea mtu ambaye hufanya matendo kwa njia ambayo humheshimu Mungu na kuonyesha jinsi Mungu alivyo. "Utauwa" ni sifa ya tabia ya kumheshimu Mungu kwa kufanya mapenzi yake.

Mtu ambaye ana tabia ya kiutauwa ataonyesha matunda ya Roho Mtakatifu, kama vile upendo, furaha, amani, uvumilivu, upole na kiasi.

Sifa ya utauwa inaonyesha ya kwamba mtu ana Roho Mtakatifu na anamtii.

Mapendekezo ya Tafsiri

Msemo "watauwa" unaweza kutafsiriwa kama "watu wenye utauwa" au "watu ambao wanamtii Mungu"