sw_tw/bible/kt/god.md

838 B

Mungu

Ufafanuzi

Katika Biblia, msemo "Mungu" una maana ya kiumbe wa milele ambaye aliumba ulimwengu bila chochote. Mungu alikuwepo kama Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu. Jina binafsi la Mungu ni "Yahwe".

Mungu mara zote alikuwepo; alikuwepo kabla ya kitu chochote kuwepo, na ataendelea kuwepo milele.

Yeye ni Mungu mmoja wa kweli na ana mamlaka juu ya kila kitu ulimwenguni.

Mungu ana haki timilifu, hekima isiyo na mwisho, mtakatifu, bila dhambi, wa haki, wa rehema, na upendo.

Ni Mungu wa kutunza agano, ambaye hutimiza ahadi zake daima.

Watu waliumvwa kumwabudu Mungu na ni yeye pekee wanaopaswa kumwabudu.

Mungu alifunua jina lake kama "Yahwe" ambayo ina maana ya "yeye ni" au "Mimi ni" au "Yule anayekuwepo daima".

Biblia pia hufundisha kuhusu "miungu" wa uongo ambao ni sanamu wasioishi ambao watu huabudu kwa makosa.