sw_tw/bible/kt/gift.md

929 B

zawadi

Ufafanuzi

Msemo "zawadi" una maana ya kitu chochote ambacho hupewa au kutolvwa kwa mtu. Zawadi inatolewa bila matarajio ya kurudishiwa kitu chochote.

Pesa, chakula, mavazi, au vitu vingine zitolewazo kwa watu maskini zinaitwa "zawadi".

Katika Biblia, sadaka itolewayo kwa Mungu pia hujulikana kama zawadi.

Zawadi ya wokovu ni kitu ambacho Mungu anatupatia kupitia imani kwa Yesu.

Katika Agano Jipya, msemo "zawadi" pia hutumika kumaanisha uwezo maalumu wa kiroho ambao Mungu hutoa kwa Wakristo wote kutumikia watu wengine.

Mapendekezo ya Tafsiri

Msemo wa jumla wa "zawadi" unaweza kutafsiriwa na neno au msemo ambao una maana ya "kitu ambacho kinatolewa".

Katika muktadha wa mtu kuwa na zawadi au uwezo maalumu ambao unatoka kwa Mungu, msemo "zawadi kutoka kwa Roho" unaweza kutafsiriwa kama "uwezo wa kiroho" au "uwezo maalumu kutoka kwa Roho Mtakatifu" au "kipaji maalumu cha kiroho ambacho Mungu ametoa"