sw_tw/bible/kt/gentile.md

834 B

Mataifa

Ufafanuzi

Msemo "mataifa" una maana ya mtu yeyote ambaye sio Myahudi. Watu wa mataifa ni watu ambao sio uzao wa Yakobo.

Katika Biblia, msemo "kutotahiriwa" pia hutumika kitamathali kumaanisha watu wa Mataifa kwa sababu wengi wao hawakutahiri watoto wao wa kiume kama Waisraeli walivyofanya.

Kwa sababu Mungu aliwachagua Wayahudi kuwa watu maalumu, walifikiria juu ya watu wa mataifa kama watu wa nje ambao wasingeweza kuwa watu wa Mungu.

Wayahudi pia waliitwa "Waisraeli" au "Waebrania" katika vipindi tofauti vya historia. Waliwajua wengine wote kama "watu wa Mataifa".

Watu wa mataifa pia inaweza kutafsiriwa kama "asiye Myahudi" au "asiye Muisraeli" (Agano la Kale).

Kitamaduni, Wayahudi hawakula na watu wa mataifa au kujihusishanao, ambapo mara ya kwanza ilisababisha matatizo miongoni mwa kanisa la kwanza.