sw_tw/bible/kt/fulfill.md

795 B

timiza

Ufafanuzi

Msemo "timiza" una maana ya kukamilisha au fanikisha jambo ambalo lilitarajiwa.

Pale ambapo unabii unatimizwa, ina maana ya kwamba Mungu alisababisha itokee kile kilichotabiriwa katika unabii.

Kama mtu anatimiza ahadi au kiapo, ina maana ya kwamba anafanya kile alichoahidi kufanya.

Kutimiza jukumu ina maana kufanya kazi ambayo ulipangiwa au unapaswa kufanya.

Mapendekezo ya Tafsiri

Kulingana na muktadha, "timiza" unaweza kutafsiriwa kama "fanikisha" au "kamilisha" au "kusababisha kutokea" au "kutii" au "kutenda".

Msemo "imetimizwa" inaweza kutafsiriwa kama "imekuwa kweli" au "imetokea".

Njia za kutafsiri "timiza" kama vile "timiza huduma yako" inaweza kujumuisha, "maliza" au "fanya" au "mazoezi" au "tumikia watu wengine kama vile Mungu amekuita kufanya"