sw_tw/bible/kt/foolish.md

1.1 KiB

mpumbavu, upumbavu, upuuzi

Ufafanuzi

Msemo "mpumbavu" una maana ya mtu ambaye mara kwa mara hutengeneza uchaguzi mbaya, haswa kuchagua kutokutii. Msemo "upumbavu" unaelezea mtu au tabia ambayo siyo ya hekima.

Katika Biblia, msemo "mpumbavu" mara kwa mara una maana ya mtu ambaye haamini au kumtii Mungu. Mara nyingi hii hutofautishwa na mtu mwenye hekima, ambaye humwamini Mungu na kumtii.

Katika Zaburi, Daudi anaelezea mtu mpumbavu kama mtu ambaye hamwamini Mungu, ambaye hupuuza ushahidi wote wa Mungu na uumbaji wake.

Kitabu cha Agano la Kale cha Mithali pia hutoa maelezo mengi ya mpumbavu ni nani, mtu mpumbavu yukoje.

Msemo "upuuzi" una maana ya tendo ambao sio la hekima kwa sababu ni kinyume na mapenzi ya Mungu. Mara nyingi "upuuzi" pia hujumuisha maana ya kitu ambacho ni cha kudharaulika au hatari.

Mapendekezo ya Tafsiri

Msemo "mpumbavu" unaweza kutafsiriwa kama "mtu mpumbavu" au "mtu asiye na hekima" au "mtu asiyejitambua" au "mtu asiyemcha Mungu"

Njia za kutafsiri "mpumbavu" zinawvza kujumuisha "upungufu wa uelewa" au "kutokuwa na hekima" au "kutojitambua".