sw_tw/bible/kt/faithful.md

927 B

mwaminifu, uaminifu

Ufafanuzi

Kuwa "mwaminifu" kwa Mungu ina maana kuwa na desturi ya kuishi kulingana na mafunzo ya Mungu. Ina maana ya kuwa mwaminifu kwake na kumuamini. Hali ya kuwa mwaminifu ni "uaminifu".

Mtu ambaye ni mwaminifu anaweza kuaminiwa kuweza kushika ahadi zake na kutimiza majukumu yake daima kwa watu wengine.

Mtu mwaminifu huvumilia katika kutenda kazi, hata pale ambapo ni ndefu au ngumu.

Uaminifu kwa Mungu ni matendo ya daima ya kutenda ambacho Mungu anatutaka kufanya.

Mapendekezo ya Tafsiri

Katika muktadha nyingi, "mwaminifu" inaweza kutafsiriwa kama "uaminifu" au "kujitolea" au "kutegemea".

Katika muktadha zingine, "mwaminifu" inaweza kutafsiriwa kwa neno au msemo ambao una maana ya "kuendelea kuamini" au "kuvumilia katika kuamini na kumtii Mungu".

Njia ambazo "uaminifu" inaweza kutafsiriwa inaweza kumaanisha "kuvumilia katika kuamini" au "uaminifu" au "kuamini na kumtii Mungu".