sw_tw/bible/kt/exhort.md

934 B

shawishi, ushawishi

Ufafanuzi

Msemo "shawishi" una maana ya kumsihi mtu kwa nguvu na kumbembeleza mtu kufanya kilicho sahihi. Aini hii ya kusihi inaitwa "kushawishi".

Kusudi la kushawishi ni kusihi watu wengine kuepukana na dhambi na kufuata mapenzi ya Mungu.

Agano Jipya hufundisha Wakristo kujishawishi baina yao kwa upendo, sio kwa ukali au ghafula.

Mapendekezo ya Tafsiri

Kulingana na muktadha, "kushawishi" pia inaweza kutafsiriwa kama "kubembeleza kwa nguvu" au "kusihi" au "kushauri".

Hakikisha tafsiri ya msemo huu hainyoeshi ya kuwa anayeshawishi ana hasira. Msemo unatakiwa kuonyesha nguvu na uzito, lakini usionyeshe kauli ya ukali.

Katika muktadha nyingi, msemo "shawishi" unatakiwa kutafsiriwa tofauti na "kutia moyo" ambayo ina maana ya kutia msukumo, aminisha, au kufariji mtu.

Mara kwa mara msemo huu pia unatafsiriwa tofauti na "onya" ambayo ina maana ya kuonya au kusahisha mtu kwa tabia yake mbaya.