sw_tw/bible/kt/elect.md

2.1 KiB

Aliyechaguliwa, chagua, watu waliochaguliwa, Aliyechaguliwa, Mteule

Ufafanuzi

Msemo, "wateule" una maana ya "waliochaguliwa" au "watu waliochaguliwa" na una maana ya wale ambao Mungu amewateua au chagua kuwa watu wake. "Aliyechaguliwa" au "Aliyechaguliwa na Mungu" ni jina ambalo lina maana ya Yesu, ambaye ni Masihi aliyechaguliwa.

Msemo "chagua" una maana ya kuchagua kitu au mtu au kuamua jambo. Mara kwa mara hutumika kumaanisha Mungu kuteua watu wawe wake na wamtumikie.

"Kuchaguliwa" ina maana ya "kuchaguliwa" au "kuteuliwa" kuwa au kufanya jambo.

Mungu alichagua watu kuwa wasafi, kutengwa kando na yeye kwa kusudi la kuzaa matunda mema ya kiroho. Hiyo ni sababu kwa nini wanaitwa "wateule" au "waliochaguliwa".

Msemo "aliyechaguliwa" hutumika mara nyingine katika Biblia kumaanisha baadhi ya watu kama Musa na Mfalme Daudi ambao Mungu aliwateua kama viongozi wa watu wake. Pia inatumika kumaanisha taifa la Israeli kama watu waliochaguliwa na Mungu.

Msemo "wateule" ni msemo wa zamani ambao humaanisha "waliochaguliwa" au "watu waliochaguliwa". Msemo huu katika lugha asili ni wingi inapomaanisha waumini wa Kristo.

Katika tafsiri za Biblia ya Kingereza za zamani, msemo "mteule" unatumika pote katika Agano la Kale na Jipya kutafsiri neno kwa ajili ya "waliochaguliwa". Tafsiri zaidi za kisasa hutumia "mteule" katika Agano Jipya pekee, kumaanisha watu ambao wameokolewa na Mungu kupitia imani kwa Yesu. Kwingineko katika Biblia, wanatafsiri neno hili kwa uwazi zaidi kama "waliochaguliwa".

Mapendekezo ya Tafsiri

Ni bora kutafsiri "mteule" kwa neno au msemo ambao una maana ya "waliochaguliwa" au "watu waliochaguliwa". Hizi zinaweza kutafsiriwa kama "watu ambao Mungu amechagua" au "wale ambao Mungu ameteua kuwa watu wake".

Msemo, "ambao wamechaguliwa" unaweza kutafsiriwa kama "ambao wameteuliwa" au "ambao waliteuliwa" au "ambao Mungu amewachagua".

"Ninakuchagua" inaweza kutafsiriwa kama, "ninakuteua" au "ninakuchagua".

Kwa kulinganisha na Yesu, "Aliyeteuliwa" inaweza pia kutafsiriwa kama, "Aliyechaguliwa na Mungu" au "Masihi aliyeteuliwa mahsusi na Mungu" au "Yule ambaye Mungu alimteua"