sw_tw/bible/kt/daughterofzion.md

874 B

Binti Sayuni

Ufafanuzi

"Binti Sayuni" ni njia ya kitamathali inayomaanisha watu wa Israeli. Inatumika haswa katika unabii.

Katika Agano la Kale, "Sayuni" hutumika sana kama jina jingine la mji wa Yerusalemu.

"Sayuni" na "Yerusalemu" zote zina maana ya Israeli.

Msemo "Binti" ni msemo wa ubembelezi au mapenzi. Ni sitiari ya uvumilivu na utunzaji ambao Mungu anao kwa watu wake.

Mapendekezo ya Tafsiri

Njia za kutafsiri hili yaweza kuwa, "binti yangu wa Israeli, kutoka Sayuni" au "watu kutoka Sayuni, ambao ni kama binti kwangu" au "Sayuni, watu wangu wapendwa Israeli".

Ni vyema kubaki na msemo "Sayuni" katika usemi huu kwa maana unatumika mara nyingi katika Biblia. Maandishi yanaweza kuwekwa katika tafsiri kuelezea maana yake ya kitamathali na matumizi ya kinabii.

Ni bora kukaa na msemo "Binti" katika tafsiri ya usemi huu, ikiwa inaeleweka kwa sahihi.