sw_tw/bible/kt/circumcise.md

677 B

Tohara

Ufafanuzi

Tohara ni kitendo cha kukata govi la mwanaume au mtoto wa kiume. Sherehe ya tohara hufanyika pamoja na tendo hili.

  • Mungu alimuamuru Abrahamu awatahiri wanaume wote katika familia yake na watumishi wake kama ishara ya agano lao na Mungu.
  • Mungu aliamuru uzao wa Abrahamu waendelee kufanya hivi kwa kila mtoto wa kiume katika nyumba hiyo.
  • "Kutahiri moyo" ni mitendo cha kuondoa uovu wa mtu.
  • Kwa namna ya kiroho "aliyetahiriwa" ni mtu ambaye ametakaswa na Mungu toka kwenye dhambi kupitia damu ya Yesu.
  • "Wasiotairiwa" ni watu ambao hawajatahiriwa kimwili. Pia yaweza kuwa na maana ya ambao hawajatahiriwa kiroho wasiokuwa na mahusiano na Mungu.