38 lines
1.8 KiB
Markdown
38 lines
1.8 KiB
Markdown
# 25. Shetani Anamjaribu Yesu
|
|
|
|
![OBS Image](https://cdn.door43.org/obs/jpg/360px/obs-en-25-01.jpg)
|
|
|
|
Mara tu Yesu alipokwisha kubatizwa, Roho Mtakatifu alimwongoza Yesu nyikani, huko alifunga siku arobaini mchana na usiku. kisha Shetani alifika kumjaribu Yesu ili atende dhambi.
|
|
|
|
![OBS Image](https://cdn.door43.org/obs/jpg/360px/obs-en-25-02.jpg)
|
|
|
|
Shetani alimjaribu Yesu akisema; "Kama wewe ni mwana wa Mungu yaamuru mawe haya yawe mikate upate kula".
|
|
|
|
![OBS Image](https://cdn.door43.org/obs/jpg/360px/obs-en-25-03.jpg)
|
|
|
|
Yesu akajibu; "Imeandikwa katika neno la Mungu, watu hawahitaji mkate pekee ili wapate kuishi, bali wanahitaji kila neno linalosemwa na Mungu".
|
|
|
|
![OBS Image](https://cdn.door43.org/obs/jpg/360px/obs-en-25-04.jpg)
|
|
|
|
Kisha Shetani alimchukua Yesu mpaka juu ya mnara wa hekalu na kumwambia; "Kama wewe ni Mwana wa Mungu jirushe mwenyewe chini, kwa vile imeandikwa, Mungu atakuagizia malaika wake wakuchukue ili usijigonge mguu wako katika jiwe".
|
|
|
|
![OBS Image](https://cdn.door43.org/obs/jpg/360px/obs-en-25-05.jpg)
|
|
|
|
Lakini Yesu alimjibu Shetani kwa kunukuu Maandiko akisema; " Katika neno la Mungu, anaagiza watu wake, usimjaribu Bwana Mungu wako".
|
|
|
|
![OBS Image](https://cdn.door43.org/obs/jpg/360px/obs-en-25-06.jpg)
|
|
|
|
Kisha Shetani alimwonyesha Yesu falme zote za ulimwengu na fahari zake zote na akasema; "Nitakupa hivi vyote iwapo utanisujudia na kuniabudu mimi".
|
|
|
|
![OBS Image](https://cdn.door43.org/obs/jpg/360px/obs-en-25-07.jpg)
|
|
|
|
Yesu akajibu; ondoka kwangu Shetani! Katika neno la Mungu ameagiza, "Mwabudu Bwana Mungu wako na kumtumikia Yeye peke yake".
|
|
|
|
![OBS Image](https://cdn.door43.org/obs/jpg/360px/obs-en-25-08.jpg)
|
|
|
|
Yesu hakujitia chini ya majaribu ya Shetani, hivyo Shetani aliondoka akamwacha. kisha malaika walikuja na kumhudumia Yesu.
|
|
|
|
_Simulizi ya Biblia Kutoka: Mathayo 4:1-11;_
|
|
|
|
_Marko 1:12-13; Luka 4:1-13_
|